.

.

NINI NIFANYE BOMU LIKILIPUKA

ZePLAN | 03:01:00 | 0 comments

Habari ndugu wasomaji
Matumaini yangu wote niwazima waafya.
wengi wetu huwa tunashahuku ya kujifunza na pia kutaka kujua nini mtu anapaswa afanye bomu linapolipuka na ikiwa wewe ni miongoni mwa watu waliokuwepo kwenye eneo la mlipuko.

Kwanza tujiulize swali  bomu ni nini?
Kwaufupi bomu ni silaha  ambayo hutumika kwa ajili ya kuua au kutawanya watu kipindi cha ghasia.

Kunauwezekano wakuwepo tafasiri nyingi sana lakini kwa tafasiri hiyo hapo juu inajitosheleza kabisa kueleza maana ya bomu,
Kuna aina tofauti tofauti ya mabomu kuundwa kwake kunategemea na shughuli gani bomu hilo linaenda kuianya, kuna mabomu ya aina tofauti kama vile mabomu ya machozi,nyuklia na mengine mengi
Mabomu ya machozi haya hutumika kwa ajili ya shughuli za kutawanya watu sehemu yenye ghasia mara nyingi hutumiwa na polisi pindi panapotokea vurugu za kawaida, kuna aina nyingine ya mabomu ambayo husababisha  mlipuko na kurusha vipande ambavyo huwa na adhali kubwa kwa binadamu ikiwa kuwajeruhi watu na wakati mwingine hupelekea kifo au vifo vya watu.

Nini nifanye bomu likilipuka
Chakwanza unaposikia mlipuko wa bomu unashauriwa alale chini.
kwasababu bomu linapolipuka hurusha vipande vipande ambavyo husababisha majeraha kwa mtu nakupekea ulemavu na wawakati mwinine vipande hivyo hupelekea  kifo ,kulala chini itamsaidia mtu kuepukana na vipande hivyo ambavyo huruka juu mita kadhaa baada ya bomu kulipuka mara nyingi watu wengi wanao lala chini huwa salama
marachache sana na kwa bahati mbaya kama bomu litalipukia ndani ya jengo mtu anaweza kuadhirika kutokana na vipande hvyo kupiga ukuta na kuanguka na kujeruhi watu walio kuwa wamelala chini.wakati mwingine vifo hutokana na kuangukiwa na kitu kama ukuta au vitu ambavyo hudondoka kutokana na kishindo cha bomu.
Kwahiyo kwa kipindi hiki ambacho tunakabiliwa na vitisho vya ugaidi imenilazimu nitoe elimu hii ndogo kwako ili na wewe uwafikishie wengine kama ndugu,jamaa,marafiki na watu wengine wote,nitajisikia furaha sana kama utafikisha somo hili, lengo ni kuokoa maisha ya watu wanaotuzunguka

Kutokana na vitisho vya ugaidi hatua ya tahadhari ni lazima ichukuliwe ,kwakipindi hiki haishauriwi ukae kwenye mikusanyiko ya watu,
Magaidi huwa wanalenga maeneo yenye mkusanyiko ya  watu  wengi maranyingi zaidi kwahiyo kuwepo kwako kwenye mikusanyiko hiyo itakupelekea uwe kwenye hatari.
Hata hivyo mwananchi yeyote unashauriwa  kutoa taarifa polisi pindi uonapo mtu ambae unahisi simtu mzuri kwenye maeneo yanayo kuzunguka kwa haraka iwezekanavyo Tanzania ni yetu sote na nijukumu letu kuilinda niwatakie mapumziko mema
imeletwa kwenu na
A.F. Ngoma

Mungu ibariki Africa ,Mungu ibariki Tanzani

Unaweza ukachangia kwa kutoa maoni yako au ukasema unachokijua kuhusu Bomu kupitia
ochec54@gmail.com

Call:+255 657 19 9199

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments