BOKO HARAM WAWAGUMZO DAVID MILIBAND ALIA NAO
Waziri wa zamani wa
mambo ya nje wa Uingereza, David Miliband, amesema kwamba mgogoro wa
kibinaadamu ambao unasababishwa na kundi la wapiganaji wa Boko Haram,
kaskazini mashariki mwa nchi ya Nigeria haupewi uzito unaostahili na
jamii ya kimataifa.
Miliband ametoa kauli hiyo wakati alipofanya ziara katika maeneo ya Kanda ya Kaskazini Mashariki nchini Nigeria.
Milliband ni rais wa kamati ya kimataifa ya uokozi, moja ya vitengo adimu vinavyotoa huduma ya misaada ya kibinaadamu na kusaidia watu waliopoteza makaazi yao kutokana na ghasia.
Katika ziara hiyo, Milliband alikutana na watu waliokimbia makazi yao wakiwemo watoto wenye matatizo kadhaa, wengine ni wanigeria waliolazimika kuwa wakimbizi baada ya kufukuzwa kwa nguvu kutoka nchini Cameroun hivi karibuni.
Bwana Miliband alionyesha wasiwasi wake juu ya kile alichokiita usiri ulioko eneo hilo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Inakadiriwa kuwa watu milioni tatu hawana makaazi katika kipindi cha miaka sita ya waasi hao wa Boko Haram ambao wamekwisha ua karibu watu elfu ishirini.
Miliband aliyasema haya alipokuwa akizungumza haya katika ziara yake.
Category:
0 comments