.

.

IRAQ:VIKOSI VYA SERIKALI VIKISHIRIKIANA NA VIKOSI VYA KIKABILA KUPAMBANA VYAKOMBOA MJI WA RAMADI

ZePLAN | 11:57:00 | 0 comments



Mamlaka nchini Iraq inasema kuwa vikosi vya serikali vimeanzisha mashambulizi makali ya kukomboa eneo la katikati mwa mji wa Ramadi, ambalo limekuwa chini ya udhibiti wa wapiganaji wa Islamic State tangu mwezi wa Mei.

Maafisa wa Iraq wanasema kuwa vikosi vya serikali vikiungwa mkono na vikosi vya kikabila pamoja na mashambulizi ya angani kutoka kwa vikosi vya muungano vinavyoongozwa na Marekani, vimefanikiwa tangu mwanzo wa mashambulizi hayo yalioanza usiku wa manane.

Serikali ya Iraq imefanya ukombozi wa mji wa Ramadi kuwa lengo kuu.

 
Imekuwa ikijitayarisha kwa miezi kadha, kukata njia za usambazaji wa bidhaa, na mara kwa mara, kuwataka wenyeji mjini humo kuhama.
Swala hilo limekuwa kikwazo kikuu, kwani watu wengi wamesalia mjini humo, na kutatiza mashambulizi ya angani yanayotekelezwa na vikosi vya muungano .

Inakadiriwa kuwa mamia ya wapiganaji wa Islamic State wamesalia Ramadi.

 
 
Maafisa wa Iraq wanasema kuwa vikosi vya serikali vinaungwa mkono na vikosi vya kikabila
Ripoti kutoka huko zinasema wamekuwa wakijaribu kutuliza uasi dhidi yao, na pia kuwazuia raia kuondoka.
Mamalaka nchini Iraq inasema kuwa vikosi vya kikabila vimejiunga na mashambulizi ya kukomboa mji huo, na kusema kuwa huenda wakaukomboa mji huo ifikapo mwishoni mwa wiki hii.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments