KENYA:ZIARA ZA RAIS UHURU KENYATTA ZAZUA GUMZO NCHINI KENYA
Picha ni Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta
amefanya ziara 43 nje ya nchi tangu kuingia madarakani miaka mitatu
iliyopita na Alhamisi wiki hii anatarajiwa kuzuru Kigali, Rwanda.
Ziara hizi zimeonekana kuwakera wananchi wengi ambao wameingia kwenye mitandao ya kijamii kuzikosoa.Kwa takriban siku mbili, jumbe za kukejeli safari hizo zimekuwa mada kuu katika mitandao ya kijamii, Wakenya wakitumia kitambulisha mada #UhuruInKenya.
Wanalinganisha kurejea kwa Rais Kenyatta nchini Kenya kutoka Afrika Kusini na ziara zilizofanywa na viongozi mashuhuri duniani kama vile Rais Barack Obama mwezi Julai na Papa Francis mwezi Novemba. Vitambulisha mada vilivyotumiwa wakati huo vilikuwa #ObamaInKenya na #PopeInKenya.
Bw Kenyatta amefanya ziara 43 katika muda ambao amekuwa uongozini, ambazo zinazidi ziara 33 za nje ya nchi alizofanya mtangulizi wake Rais mstaafu Mwai Kibaki miaka kumi aliyokuwa mamlakani.
Category:
0 comments