MAREKANI:MMAREKANI ALIE JIUNGA NA AL-SHAABABU ATIWA NGUVUNI
Raia wa Marekani ambaye alijiunga na kundi la wapiganaji wa Kiislamu wa al-Shabaab nchini Somalia amekamatwa.
Afisa
wa serikali ya Somalia amesema kwamba Mwamerika huyo alikamatwa na
wanajeshi kusini magharibi mwa Mogadishu akiwatoroka wapiganaji pinzani
wa Kiislamu.Hii ni baada ya wenzake kuuawa kwenye vita vya kambi pinzani ndani ya kundi hilo.
Mkuu wa wilaya ya Barawe Hussein Barre Mohamed amesema ingawa mwanamume huyo amekuwa Somalia kwa muda mrefu, hakuweza kuzungumza Kisomali.
Kundi la Al-Shabab huegemea mtandao wa al-Qaeda, lakini baadhi ya makundi yamehama na kujiunga na kundi linalojiita Islamic State.
Category:
0 comments