.

.

MMBUNGE MMOJA AFARIKI NCHINI KUWAIT AKIWA AMEKALIA KITICHAKE BUNGENI

ZePLAN | 10:22:00 | 0 comments

 
Mbunge mmoja nchini Kuwait amefariki katika kikao cha bunge.
Video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii imeonyesha mbunge huyo bwana Nabil al-Fadl aliye na umri wa miaka 65 akianguka kwa ghafla kutoka kwenye kiti chake.

Wabunge walimzingira, kisha waziri wa afya (Dr Ali al-Obaidi) akijaribu kumtibu hadi wakati madaktari walipowasili.

Marehemu bwana Al-Fadl -- ambaye alikuwa ni mwandishi wa habari alikuwa maarufu kwa kutumia jarida lake kuwaasa wabunge wenza na hata wakati mwengine kuwakashifu.

Aidha Al-Fadl alifahamika zaidi kwa kuwakaripia waasi wa kiislamu ambao aliwashambulia kwa maneno makali .

Wakati mmoja aliwashangaza wasomaji wake alipoitaka serikali iondoe mara moja marufuku ya uuzaji wa pombe na maeneo ya burudani.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments