.

.

RAIS WA TANZANIA JOHN POMBE MAGUFULI AMTUMBUA JIPU AFISA MKUU WA RELI

ZePLAN | 14:51:00 | 0 comments


 
Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemsimamisha kazi mkurugenzi mkuu wa kampuni ya reli Tanzania (RAHCO) Benhadard Tito.

Mhandisi Tito amelazimishwa kukaa kando ilikufanikisha uchunguzi katika utaratibu uliotumika wakati wa utoaji wa zabuni ya ujenzi wa reli ya kati.

 Rais Magufuli alichukua hatua hiyo kali baada ya mkutano na wadau wanaohusika na ujenzi wa reli ya kisasa yaani “Standard Gauge”

Uchunguzi wa kimsingi unaelekezwa kwa utoaji wa zabuni hiyo inayokisiwa kugharimu takriban dola milioni $14.


Si hao tu walioathirika na amri hiyo ya rais Magufuli, bodi ya Mamlaka ya Reli Tanzania (TRL) pia imevunjiliwa mbali. 
 
Sasa Magufuli al maarufu "The Bulldozer" ameiagiza mamlaka ya udhibiti wa manunuzi ya umma (PPRA) kuchunguza na kuchukua hatua dhidi ya kampuni za ukandarasi zilizopewa zabuni ya ujenzi huo endapo itathibitika kuwa zimeshiriki katika ukiukwaji wa sheria.

Si hao tu walioathirika na amri hiyo ya rais Magufuli, bodi ya Mamlaka ya Reli Tanzania (TRL) pia imevunjiliwa mbali.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments