KAMANDA WA IS ANUSURIKA KIFO KWENYE SHAMBULIZI LA WAMEREKANI
Kundi moja la wachunguzi linasema
kuwa kamanda mmoja wa ngazi za juu wa kundi la Islamic State alijeruhiwa
vibaya lakini hakuuawa katika shambulio la angani lililotekelezwa hivi
karibuni kaskazini mashariki mwa Syria.
Lakini kundi la wachunguzi hao nchini Syria lililo na makao yake makuu nchini Uingereza limesema kuwa lina habari kwamba alichukuliwa na kupelekwa kupata matibabu mjini Raqqa.
Hakuna tamko lolote kutoka kwa IS kuhusu ripoti hiyo ya kifo cha Shishani.
Mwaka uliopita ,Marekani ilitowa zawadi ya dola milioni 5 kwa yeyote yule ambaye angetoa habari za Shishani ambaye inasema ameshikilia nyadhfa kadhaa katika kundi hilo ikiwemo uwaziri wa vita.
Category:
0 comments