.

.

KOREA KASKAZINI KUJARIBISHA TENA MABOMU YA NYUKLIA YALIOTENGENEZWA NA WANASAYANSI NCHINI HUMO

ZePLAN | 01:07:00 | 0 comments

Rais Kim Jong Un 
 
Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-Un ameamrisha majaribio zaidi ya kinyukilia yakitumia mabomu yasiyokuwa na nguvu, ambayo anasema wanasayansi wa nchi yake wametengeneza.

Shirika la utangazaji nchini limetangaza kwamba Kim alitoa amri hiyo baada ya kushuhudia uzinduzi wa makombora mengine hapo Alhamisi.

Awali kiongozi huyo alisema wanasayansi wa nchi yake wamefanikiwa kupunguza ukubwa na mabomu ili yaweze kuwekwa kwenye makombora.
 
Waandishi wa habari wamesema ikiwa hili litathibitishwa, hii itakua tishio kubwa kwa Korea Kusini na nchi nyingine zilizoko kwenye kanda hiyo.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments