Marekani imewaonya raia wake walio
Ulaya na wanaopanga kuzuru bara hilo kuhusu uwezekano wa kutokea kwa
mashambulio mengine ya kigaidi.
Tahadhari hiyo imetolewa baada ya mashambulio kuua watu 34 katika mji wa Brussels Jumanne.
Wizaya ya mashauri ya kigeni ya Marekani imesema makundi ya kigaidi huenda yakatekeleza mashambulio karibuni.
“Makundi
ya kigaidi yanaendelea kupanga mashambulio ya kuteketelezwa karibuni
kote Ulaya, yakilenga hafla za michezo, maeneo ya kitalii, migahawa na
uchukuzi,” taarifa ya wizara hiyo ilisema.
Raia wa Marekani
wanaozuru Ulaya wametakiwa kuwa macho zaidi maeneo yenye watu wengi au
wanapotumia mifumo ya uchukuzi wakati wa sikukuu ya Pasaka.
Miji mingi Marekani imeimarisha ulinzi katika viwanja vya ndege na vituo vya treni na mabasi.
Serikali hata hivyo imesema bado haina habari za uhakika kuhusu uwezekano wa kutokea kwa mashambulio Marekani.
Washukiwa wanaodaiwa kutekeleza shambulio uwanja wa ndege wa Zaventem Kundi linalojiita Islamic State (IS) limedai kuhusika katika mashambulio Brussels.
Taarifa
iliyopakiwa mtandaoni na kundi hilo ilisema maeneo hayo
yaliyoshambuliwa “yaliteuliwa kwa umakinifu mkubwa” na kuonya kuwa
kutatokea mabaya zaidi kwa mataifa yanayopinga kundi la Islamic State.
Category:
About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!
Related posts:
If you enjoyed this article, subscribe to receive more just like it.
0 comments