.

.

TRUMP ATABIRI KUHUSU KUZUKA KWA FUJO NCHINI MAREKANI

ZePLAN | 23:57:00 | 0 comments

Trump
 Trump ameshindwa katika mchujo jimbo la Ohio  
 

Mfanyabiashara tajiri Marekani Donald Trump, amesema anafikiri kutatokea fujo iwapo ataongoza kwa wajumbe kisha chama chake cha Republican kitakosa kumuidhinisha awanie urais.

Bw Trump alishinda mchujo katika majimbo matatu zaidi, likiwemo jimbo la Florida mnamo Jumanne, ingawa alishindwa katika jimbo jingine muhimu la Ohio.

Hatua yake ya kushindwa Ohio huenda ikawawezesha wahafidhina wadhibiti wa chama cha Republican, ambao hawajafurahishwa na mtazamo wake, kumpendekeza mgombea mwingine kwenye mkutano mkuu wa kuidhinisha wagombea Julai.

Trump Mfuasi wa Donald Trump
Hayo yakijiri, Bw Trump amesema hatashiriki mdahalo katika runinga ya Fox News wiki ijayo akisema ametoshena na midahalo.

Katika chama cha Democratic, Hillary Clinton ameimarisha uongozi wake na kumshinda mpinzani wake wa pekee Bernie Sanders katika majimbo manne yaliyofanya mchujo Jumanne.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments