Waendesha mashtaka
nchini Marekani wanasema kuwa aliyekuwa spika wa bunge la wawakilishi,
Denis Hastert, alikubali kulipa dola milioni tatu na nusu kisiri, ili
kuficha kuhusika kwake na unyanyazaji wa kingono dhidi ya wavulana
kadhaa.
Katika nyaraka zilizowasilishwa mbele ya mahakama siku ya
Ijumaa, waendesha mashtaka hao wanasema fedha hizo zililipwa kwa mtu
ambaye alikuwa na umri wa miaka kumi na minne wakati alipodhulumiwa
miongo kadhaa iliyopita.
Aliyekuwa spika wa bunge la Marekani Kulia Denis Hastert akiwa na rais wa zamani Bush
Oktoba mwaka uliopita, spika huyo wa zamani alikiri kuwa alivunja sheria za benki kwa kumlipa fidia mtu mmoja ambaye hakutajwa. Wanasema
bwana Hastert ambaye ana umri wa miaka 74, aliwadhulumu kimapenzi
wavulana wengine watatu wakati alipokuwa kocha wa mieleka kabla ya
kujiunga na siasa. Hastert atahukumiwa baadaye mwezi huu.
Category:
About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!
Related posts:
If you enjoyed this article, subscribe to receive more just like it.
0 comments