.

.

ADAM BARROW AKABIDHIWA KITI CHA URAIS GAMBIA TAZAMA VIDEO HAPA

ZePLAN | 01:25:00 | 0 comments

Adama Barrow, left, is sworn in as president of the Gambia. 
Adama Barrow, aliyeibuka mshindi katika uchaguzi wa urais nchini Gambia ameapishwa rasmi kuwa rais wa taifa hilo.

Alikula kiapo hicho katika ubalozi wa Gambia nchini Senegal huku akiwaagiza wanajeshi wa Gambia kusalia katika kambi zao.
Ametambuliwa kimataifa.
Supporters of Adama Barrow celebrate his inauguration in Dakar.
Raia wakifurahia baada ya kupata Rais mpya

Lakini aliyekuwa rais wa taifa hilo Yahya Jammeh amekataa kujizulu na muda wake wa kuhudumu umeongezwa na bunge.
Viongozi wa Afrika Magharibi wameshindwa kumsihi bw Jammeh kuondoka mamlakani.Rais Mteule wa Gambia Adama Barrow
Rais Mteule wa Gambia Adama BarrowRais Mteule wa Gambia Adama BarrowRais Mteule wa Gambia Adama Barrow

Wametishia kumuondoa kwa nguvu.
Bw Jammeh alishindwa katika uchaguzi huo wa Disemba mosi ,kulingana na tume ya uchaguzi nchini humo.

 Lakini anataka matokeo ya uchaguzi huo kufutiliwa mbali akidai makosa mengi katika uchaguzi huo.

 ''Mimi Adama Barrow ,naapa kwamba nitatekeleza wajibu wangu katika afisi ya urais wa taifa la Gambia kwamba nitahifadhi na kutetea katiba'' .
 Na katika hotuba yake ya kuapishwa ,aliwaagiza wanachama wote wa jeshi la gambia kusalia katika kambi zao. ''Wale watakaopatikana wakibeba silaha watachukuliwa kuwa waasi'', alionya. TAZAMA VIDEO YA RAIS MPYA WAGAMBIA AKIWA KWENYE KIAPO

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments