.

.

OBAMA ATOA MSAMAHA KWA WANAJESHI

ZePLAN | 00:51:00 | 0 comments

Image result for obama
Rais Barrack Obama wa Marekani 
 
Rais Obama amebatilisha kifungo cha jela kwa Chelsea Manning, aliyekuwa mwanjeshi wa Marekani aliyehukumiwa kifungo cha miaka 35 jela kwa kosa la kufichua nyaraka za siri.
Taarifa kutoka ikulu zinasema Manning ataachiwa huru ifikapo mwezi wa tano.

Mwanajeshi huyo aliyekuwa mwanamageuzi alifanya kazi huko Iraq na alikuwa akijulikana pia kama Bradley Manning. 
Chelsea Manning awali alikana makosa yake kabla ya kukubali


Chelsea Manning awali alikana makosa yake kabla ya kukubali
Alipatikana na hatia hiyo mwaka 2013 kwa kuweka karibia robo tatu ya mamilioni ya nyaraka za siri za kijeshi na kidiplomasia katika tovuti ya WikiLeaks.

Rais Obama pia ametoa msamaha kwa mstaafu jenerali James Cartwright, aliyekubali kosa la kutoa taarifa za uongo katika uchunguzi uliokuwa ukifanywa na FBI katika udukuzi wa kompyuta kuhusu mipango ya kinyuklia ya Iran.

Category:

About GalleryBloggerTemplates.com:
GalleryBloggerTemplates.com is Free Blogger Templates Gallery. We provide Blogger templates for free. You can find about tutorials, blogger hacks, SEO optimization, tips and tricks here!

0 comments